Tuko Pamoja

Tuko Pamoja

Wednesday, September 22, 2010

Wananchi wa jiji la Mbeya wampatia ushirikiano mkubwa JOSEPH MBILINYI katika mikutano yake ya kampeni na kumuahidi ushindi wa kishindo.

 
 Akina mama wa Itende wakisalimiana na mgombea ubunge Joseph Mbilinyi
  
Wananchi wa Nsalaga wakisikiliza kwa makini katika mkutano 
    
 Mgombea wa ubunge Joseph Mbilinyi akizungumza na wananchi 

 Wananchi wa Nsalaga wakisikiliza kwa makini sera za CHADEMA jijini Mbeya 
Kulia ni mwenyekiti wa CHADEMA wilaya ya Mbeya na Wana CHADEMA akibadilishana mawazo katika moja ya mikutano ya kampeni jijini Mbeya 
Mkereketwa wa CHADEMA akiwa amebandika picha ya kampeni katika shati lake kama alivyokutwa maeneo ya Ilemi darajani huku akiwa ameshika kadi ya kupigia kura mkononi 
  

  
G SOLO akiimba pamoja na umati mkubwa wa watu katika moja ya mikutano ya kampeni za mgombea ubunge bwana Joseph Mbilinyi 
  
Akina mama hawa walisimamisha gari ya mgombea ili wampe baraka zao Joseph mbilingi ( SUGU )

Jaji Mfalila: Chagueni upinzani ASEMA MGOMBEA ATAYETOA ELIMU, AFYA BURE NDIYE ANAFAA KUWA RAIS

                                                       Jaji Mstaafu Lameck Mfalila
JAJI mstaafu wa Mahakama ya Rufaa nchini, Lameck Mfalila, amewataka Watanzania kuchagua mgombea aliyethubutu kusema; "atasomesha wanafunzi na kutoa huduma ya afya bure." Akitetea msimamo huo, Jaji Mfalila alisema:"Huyu ni shujaa, sio ghilba bali amethubutu kusema anaweza kufanya mabadiliko hayo, mchagueni."

Katika mkutano wa wanaharakati kuhusiana na Uchaguzi Mkuu jijini Dar es Salaam jana, Jaji Mfalila alitoa sifa kwa mgombea mmojawapo wa urais kutoka kambi ya upinzani ambaye ameweka wazi kwamba akiingia Ikulu, elimu na afya zitatolewa bure.

“Kuna mgombea mmoja kutoka kwenye vyama vya upinzani, naona anaitia changamoto serikali, yeye alithubutu kusema ikiwa atachaguliwa kuingia Ikulu, atasomesha wanafunzi na kutoa huduma ya afya bure, huyu ni shujaa, sio ghilba bali amethubutu kusema anaweza kufanya mabadiliko hayo, mchagueni,” alisisitiza.

Kwa mujibu wa Jaji Mfalila, ikiwa wananchi watafanya mabadiliko hayo wataweza kupata kiongozi bora atayesimamia mali asili za nchi yake vizuri.

Ingawa hakumtaja mgombea huyo, lakini wagombea urais kwa tiketi ya Chadema, Dk Willibrod Slaa na wa CUF, Prof Ibrahim Lipumba ndiyo ambao wamekuwa wakitoa ahadi hiyo ya kutoa elimu na afya bure kama wakishinda uchaguzi.

Kwa upande wa Dk Slaa, amekuwa akisema iwapo Chadema itapewa ridhaa ya kuongoza nchi, fedha zilizoporwa kifisadi zitarejeshwa na kuwa mwanzo wa kutoa elimu na afya bure kwa wananchi.

Ahadi yake hiyo ilimsababishia Dk Slaa kuingia katika mgogoro na Spika wa Bunge aliyemaliza muda wake, Samuel Sitta, aliyepinga sera ya wapinzani ya kutoa elimu bure akisema kuwa haiwezekani.

Naye Prof Lipumba mara kadhaa amenukuliwa akisema kama akichaguliwa kuwa rais katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu, Serikali yake itaondoa gharama za elimu katika ngazi zote.
Lipumba alitoa kauli hiyo hivi karibuni wakati akijinadi katika mikutano tofauti ya kampeni iliyofanyika mkoani Lindi na Mtwara.

Lipumba alisema CUF imeazimia kuweka suala la elimu ya bure katika vipaumbele vyake, kwa vile sekta hiyo ni mkombozi wa umaskini uliokithiri kwa wananchi wengi.

Katika mkutano huo wa jana, Jaji Mfalila alisema Tanzania ina kampuni kubwa ambazo zinafanya shughuli za kuzalisha madini yakiwamo ya dhahabu na almasi, jambo ambalo lingeweza kuingiza kiasi kikubwa cha fedha, lakini kutokana na ujanja uliopo makampuni hayo yanalipa kiasi kidogo cha kodi huku yakiwanufaisha wachache.

Jaji Mfalila ambaye alitumia zaidi ya saa moja kuitafakari serikali, ilipotoka, ilipo sasa na inapokwenda, alisema kuwa rasilimali zilizopo zinatumika kiujanja ujanja jambo ambalo limesababisha nchi kutegemea misaada kutoka kwa wahisani na nchi marafiki.

Alisema kutokana na hali hiyo, wananchi wanapaswa kufanya mabadiliko ya kumchagua kiongozi atakayeweza kuleta maendeleo kwenye taifa lake, hasa katika nafasi ya rais ambayo ndio injini ya maendeleo.

“Tanzania bila ya misaada inawezekana, tuna rasilimali za kutosha ambazo zikitumika vizuri zinaweza kuleta mabadiliko ya kimaendeleo. Wananchi wanapaswa kufanya mabadiliko ya kumchagua kiongozi anayeweza kuthubutu kuleta maendeleo hayo, chagueni upinzani kwa ajili ya maendeleo,” alisema Jaji Mfalila.

Jaji Mfalila alisema nchi nyingi duniani zilizopiga hatua kimaendeleo zilitumia rasilimali zake vizuri bila ya kuingiza ujanja ujanja.

Akizungumzia kilimo, Jaji Mfalila alisema kwamba inashangaza kilimo cha Tanzania mpaka sasa kinategemea mvua za misimu na pale ambapo mvua hizo hazinyeshi, viongozi wanaitana Ikulu kutafuta nchi ya kuomba msaada wa chakula wakati ardhi yenye rutuba ipo.

“Hii ni aibu ya kutosha kuona tunaomba msaada wa chakula wakati tuna ardhi bora  kwa ajili ya shughuli za kilimo, lakini bado tunasubiri mvua ya miezi mitatu ambapo isiponyesha viongozi wanaitana Ikulu kwa ajili ya kutafuta nchi ya kuomba msaada wa chakula, kweli tunahitaji mabadiliko," alisema.

Akizungumzia enzi za uongozi wa Mwalimu Julius Nyerere, Jaji Mfalila alisema wanafunzi  wa chuo kikuu waliweza kupatiwa mahitaji yote muhimu ili wasome kwa umakini zaidi, lakini siku hizi fedha za matibabu, chakula na kulipia gharama za ada zimekuwa tatizo kwao.
“Nasikia tu wanafunzi wamegoma kwa ajili ya kukosa fedha za ada, chakula na matibabu wakati enzi zetu tulikuwa tunakabidhiwa hundi ya malipo kabla ya kufika shuleni,”alisema.

Naye Profesa Chris Peter Maina, wa Shule ya Sheria ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Kituo cha Huduma ya Sheria Zanzibar, aliunga mkono kauli iliyotolewa na Jaji Mfalila akisisitiza kuwa elimu yaweza kutolewa bure.

“Nimesoma bure kuanzia darasa la kwanza hadi nilipopata shahada yangu ya uzamili. Sharti kuu lililokuwapo ni kwamba nilihitajika kujaza fomu kuazimia kuwa nitalitumikia taifa langu baada ya kuhitimu masomo yangu,” alisema Profesa huyo.Aliongeza: “Kama nisingepata elimu ya bure, leo hii ningelikuwa nachunga ng'ombe kijijini kwetu.”

Profesa Maina alisema tatizo kubwa linaloikabili Tanzania ni kwamba viongozi wamevigeuza vipaumbele juu chini kwa kuwapa wakaguzi wa elimu wanaotumia magari ya Sh 150milioni yaliyo na viyoyozi kazi ya kukagua madarasa yasiyo na madawati na yenye wanafunzi wanaoketi chini.

“Sielewi ni kwanini mpaka leo miaka 50 baada ya uhuru wanafunzi wa Tanzania bado wanaketi chini kwenye madarasa yao?” alishangaa Profesa huyo wa sheria.

Sunday, September 19, 2010

Yaliyo jili katika tamasha la uchangiaji kampeni za JOSEPH MBILINYI (SUGU)

      
 Hapa sugu na Danny Msimamo katika meza kuu
Msanii kutoka Isanga Family akifanya vitu vyake jukwaani
Wagombea wa ubunge wakizungumza mawili matatu katika stage mjini Tunduma 
 
 Mkoloni akiwapa burudani wakazi wa Tunduma 
 
 Sugu on stage ilikua babkubwa sana 
Mashabiki wa kiangalia show ya Sugu 
        Huyu Dj ni Bwana mdogo tu  lakini kazi yake ni noma hapo akiwa na G solo wabadilishana mawili matutau ili show iende kama ilivyo pangwa

Friday, September 17, 2010

Joseph Mbilinyi ataka bandari ya nchikavu Mbeya

MGOMBEA ubunge wa jimbo la Mbeya Mjini kwa tiketi ya Chadema, Joseph Mbilinyi amewaahidi wananchi wa Mbeya kuwa endapo atachaguliwa kuwa mbunge atahakikisha serikali inaweka bandari ya nchi kavu mkoani hapa ili kuwarahisishia kazi wafanyabiashara wa nje na kukuza maisha ya wakazi wa mjini hapa.

Mbilinyi, mmoja wa wasanii waliotangaza muziki wa kizazi kipya akitumia jina la Mr ll 'Sugu' alitoa kauli hiyo wakati wa kampeni zake akisema wakati umefika wakati kwa mkoa wa Mbeya kuwa na bandari ya Nchi kavu ili kuwezesha wafanyabiashara wanaotoka nchi jirani za Zambia na Malawi kupata bidhaa kirahisi mkoani hapa badala ya kusafiri hadi Dar es salaam.

Mbilinyi alisema Mbeya imekosa mkakati wa kusaidia wafanyabiashara kutoka nje kupata bidhaa zao mkoani hapa na ndio maana hupitiliza kwenda Dar es salaam kufuata bidhaa, wakati mji huu ni kiungo kikubwa cha kibiashara na nchi za Malawi na Zambia.

Alisema mfumo wa biashara mkoani hapa umekua kikwazo kwa wafanyabiashara wengi ndio maana hata wafanya biashara wa Mbeya wamekimbilia Dar es salaam kuendeleza biashara na kuutelekeza mkoa wao.

“Tukiwa na ushirikianao mzuri baina ya serikali na wafanyabiashara na kuwa na bandari ya nchikavu itasaidia wafanyabiashara kutoka Malawi, Congo, Zambia na Zimbabwe kununua bidhaa zao hapa na kuongeza mapato kwa serikali ya Mbeya,” alisema Mbilinyi.

Alisema watoto wa mkoani hapa wamekuwa wakichangishwa michango mingi kwenye shule zao kutokana na serikali ya mkoa kutokuwa na vyanzo vingi vya mapato.

Mbilinyi pia alisisitizia ahadi yake ya kuhakikisha kila shule ya Mbeya Mjini inakuwa na kompyuta 30 ambazo alisema zitapatikana kutoka kwa wafadhili ili kusaidia wanafunzi kielimu.

"Sijaja kuihubiri Chadema, bali nimekuja kukomboa Mkoa wa Mbeya na hasa jimbo la Mbeya Mjini ili kuweka heshima ya jiji kwa wakazi wake kuwa na maisha yenye kupendeza... ni aibu kuona mkoa wa mbeya unapendeza pembezoni huku katikati kukiwa na maisha mabovu kwa wananchi," alisema.

"Maendeleo hayahitaji wageni toka nje ya nchi bali kushirikiana kwa pamoja kutasaidia jamii yetu."

Thursday, September 16, 2010

Leo tulikuwa Mwansekwa nnje kidogo ya jiji la Mbeya

    
Wananchi wa Mwansekwa waki mkaribisha Mheshimiwa JOSEPH MBILINYI 
JOSEPH MBILINYI (Mr II ) aki hutubia wananchi 
Mwenyekiti wa CHADEMA Mbeya nae alikuwa na jambo la kuzungumza na wananchi 
 Hapa Mr Mbwembwe ali kua akitoa buruda ni kwa wakazi wa mwansekwa 
  
POLICE pia wali kuwepo eneo la mkutano iliku hakikisha usalama unakuwa ni wakutosha .

Wednesday, September 15, 2010

Joseph Mbilinyi na harakati zake za Ubunge Mbeya mjini

Hapa Msafara wa Joseph Mbilinyi ukipita katika jiji la Mbeya mjini
Hapa akinadiwa na Mwenyekiti wa CHADEMA Mbeya
Wananchi wakipunga mkono kudhiirisha kumkubali Sugu kuwa Mbunge wao
Makamanda wa CHADEMA wakiweka njia kwa ajili ya Sugu kupita
Moja ya Gari linatumika kwa PA katika kampeni za Sugu

Hapa Mgombea Ubunge Joseph Mbilinyi akiwasalimu wakazi wa kitongoji cha Mabatini-Mbeya Mjini

Sugu akifika eneo la mabatini

Umati wa watu waliofika kumsikiliza sugu

Mmoja wa Kamanda wa CHADEMA  akiongea na wananchi

Bwana Joseph Mbilinyi akiongea na wananchi wa Mabatini


Sunday, September 5, 2010

Maaskofu wasusia mwaliko wa JK

*Ni kushirikiana naye kula futari
Mwandishi Maalum, Mbeya

MAASKOFU wa makanisa ya Kikristo na wachungaji mkoani Mbeya walioalikwa kula futari (kufuturu) na Rais Jakaya Kikwete katika Ikulu ndogo alipokuwa katika ziara za kampeni hivi karibuni, walikataa kwa maelezo kuwa hawawezi kushiriki naye kwa kuwa ni mgombea wa urais.
Habari ilizozipata Mwananchi Jumapili zinaeleza kuwa maaskofu na wachungaji hao walimgomea Rais Kikwete Septemba Mosi, mwaka huu wakati wa ziara yake mkoani Mbeya.
Gazeti hili lilifanya juhudi kumtafuta Katibu Mkuu wa CCM, Yusuph Makamba kutoa ufafanuzi wa taaarifa hizo jana.
Hata hivyo alipopatikana kuzungumzia suala hilo Makamba alisema kwa kifupi, "hilo mimi sijui, silijui hilo".
Kwa mujibu wa mwaliko huo ambao Mwananchi Jumapili iliuona, viongozi hao walitakiwa kufika Ikulu ndogo saa 12 jioni mjini Mbeya kufuturu pamoja na Rais Kikwete.
Baada ya kupokea mwaliko huo, viongozi hao wa dini walisema kufuturu na Rais Kikwete wakati huu wa kampeni kungeweza kuvunja uaminifu wao kwa waumini kwa vile Kikwete ni sawa na wagombea wengine wa urais wanaostahili kupatiwa haki sawa.
Habari hizo zimedai kuwa mbali ya maaskofu na wachungaji wa dini mbalimbali takribani 40 walioalikwa kula futari hiyo, mwaliko huo pia uliwahusu viongozi wa dini nyingine.
Viongozi hao wa dini walisema mwaliko huo haukuwa na manufaa yoyote kwa viongozi wa kikiristo ambao hawakufunga hivyo wasingeweza kushiriki futari inayopaswa kuliwa na ndugu zao Waislamu waliofunga.
Hii ni mara ya kwanza katika uchaguzi huu viongozi wa dini kutakaa mwaliko wa rais Kikwete.
"Sisi maaskofu mkoani Mbeya ambao tulialikwa juzi (Jumanne) kwenye futari Ikulu ya Mbeya tumetafakari pamoja na wenzetu ambao hawakualikwa kuwa kitendo hiki ni rushwa ya chakula".
"Tunakilaani vikali kitendo hiki tumejiuliza kwa nini tualikwe kwa futuru sisi ambao hatuko kwenye mfungo? Tena tumechukizwa sana na mgombea, kufanyiwa zindiko uwanjani na machifu wakati amefunga," ilieleza sehemu ya waraka wa maaskofu hao kwa Mwananchi Jumapili.
Akiwa katika Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya wazee wa kimila (machifu) wa Usafwa mkoani humo walimvisha Kikwete mgolole, kumpa kiti cha kichifu pamoja na mkuki kama ishara ya kumkubali na kuahidi kuwa wananchi wote wa Mbeya watampigia kura Kikwete.
Mmoja wa Maaskofu aliyepata nafasi ya kuzungumza na Mwananchi Jumapili alisema wameugomea mwaliko huo na kuufananisha na rushwa akieleza kuwa wao hawakupaswa kualikwa kipindi hiki ambacho jamii nzima ya watanzania inawatazama viongozi wa dini na kutaka kujua wameegemea upande upi.
Askofu huyo ambaye aliomba jina lake lisitajwe kwa kuwa si msemaji wa umoja wao, alisema ni vyema viongozi wa madhehebu ya dini wakawa makini katika kipindi hiki cha kampeni.
Kwa mujibu wa mwaliko huo uliowataka waalikwa wote kuwa nadhifu waalikwa hao walitakiwa kufikisha jibu kwa mpambe wa rais Ikulu iwapo watahudhuria au la.
Askofu wa Kanisa la Pentekoste Evangelisti, Zebadia Mwanyerere Mwakatage alipohojiwa alisema kuwa hakupata mwaliko huo, lakini akasema kwamba hata angeupata asingekwenda kwa kuwa kitendo cha kualikwa na rais akiwa mgombea hakikustahili.
Mwakatage alisema ni makosa viongozi wa dini kushiriki kwenye mialiko ya wagombea uongozi na kwamba, Kikwete anatumia kofia yake akijua kuwa yeye ni mgombea sawa na wengine hali ambayo askofu huyo alisema ingempa shida iwapo angehudhuria.
Mwenyekiti wa Umoja wa Wakristo Mkoa wa Mbeya, Askofu John Mwela wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Nyanda za Juu Kusini alisema anaungana na msimamo wa maaskofu wenzake na wachungaji waliokataa kuitikia mwaliko huo kwa kuwa kwa kufanya hivyo wangekuwa wanapingana na msimamo walionao wa kutompendelea mgombea yoyote.
Askofu Mwela alisema alipatiwa kadi ya mwaliko iliyochelewa kumfikia na kwamba hata angeipata mapema asingeweza kwenda kwa kuwa hakufunga Ramadhani na kwamba, kuhudhuria hafla hiyo ingempa shida kwa waumini wake kwa vile hatakiwi kushabikia upande wowote wa siasa.
“Naunga mkono maamuzi ya wenzangu waliokataa kwenda Ikulu, kama waliliona hilo ni vyema tukawa na msimamo, tatizo huyu ni mgombea sawa na wengine na isitoshe ingekuwa tumealikwa kwenye dhifa hapo tungeenda kula chakula sio kufuturu hatukufunga sasa ningeenda kufanya nini huko,” alisisitiza Askofu Mwela.
Kiongozi huyo wa madhehebu ya kikiristo Mkoa wa Mbeya aliwataka waumini wa madhehebu hayo kuwa makini kipindi hiki cha kampeni za uchaguzi mkuu na kuwahimiza kuhudhuria kwenye mikutano ya vyama vyote kuwasikiliza wagombea ili kuchagua viongozi bora.
Askofu wa Kanisa Katoliki, Evaristo Chengula alipotafutwa kutoa maoni yake kuhusu mwaliko huo wa Ikulu ilidaiwa kuwa amesafiri nje ya mkoa huo sambamba na maaskofu wengine Alinikisa Cheyo wa kanisa la Moraviani na Thomas Daminius Kongoro wa Pentekoste Assembless Of God(PAG) wote hawakuweza kupatikana kutoa maoni yao au kuthibitisha kama walikuwa miongoni mwa waalikwa.
Umoja wa makanisa ya kikiristo unaunganisha madhehemu manne ya Jumuiya ya Kikiristo Tanzania(CCT), Makanisa ya Kikatoliki (TEC), Jumuiya ya Kipentekoste (PCT) na makanisa huru ambayo, Mwenyekiti wake ni Askofu Mwela wa Anglikani.

Thursday, September 2, 2010

KUTOKA JUKWAA LA MUZIKI MPAKA SIASA

Ni wakati wa kutoa nafasi kwa Mr II Sugu kuingia Bungeni ili kumtetea Mwananchi wa Tanzania sababu ametumia Jukwaa la Muziki kwa miaka mingi akitetea wanyonge na kukosoa pale alipoona haki aitendeki/inapindishwa.
HIVYO AHIITAJI MJADALA Mr II - SUGU ANAFAA KUINGIA MJENGONI SABABU ATAKUWA NI MOJA YA CHACHU YA KUCHOCHEA MAENDELEO KATIKA TAIFA HILI.

MWANAMUZIKI/MWANAHARAKATI MKOLONI ANYWESHWA SUMU

Mkoloni hapa akisisitiza jambo mbele ya waandishi wa habari 

Habari zilizotufikia zinaeleza kuwa Mwanamuziki na Mwanaharakati Mkoloni wa kundi la Wagosi wa Kaya ambaye ni mshirika wa karibu sana wa Mr II Sugu katika harakati zote kuanzia za muziki mpaka kwenye jukwaa la siasa, amewekewa sumu katika chakula alichokula katika moda ya Bar kubwa iliyopo eneo la Sinza Dar es salaam.


Habari hizo zimethibitisha kuwa Mkoloni ambaye kwa sasa amelazwa katika moja ya hospitali kubwa jijini alifikwa na balaa hilo alipokwenda kujipatia kifungua kinywa katika Bar hiyo na ndipo alipokutwa na dhahama hiyo ambapo baada ya kuzidiwa alikimbizwa hospitali ambapo anaendelea na matibabu.


Tukio hilo ambalo limeripotiwa polisi limeacha maswali mengi ikizingatia Mwanaharakati huyo siku za hivi karibuni amekuwa mstari wa mbele kutetea haki ya wasanii na yuko mstari wa mbele katika harakati za CHADEMA katika uchaguzi huu na pia yuko bega kwa bega na Mgombea Ubunge wa Mbeya mjini Joseph Mbilinyi hadi kwenye majukwaa ya kampeni mjini Mbeya.


HABARI KAMILI TUTAWALETEA KARIBUNI.

HISTORIA YA HARAKATI

(Uchambuzi wa Nyimbo za Mr II – SUGU)
Wimbo tunaoupitia leo unaitwa:

NI NDOTO
Mwanamuziki: Mr II - Sugu
Album: Nje ya Bongo
Mwaka: 1999

KIITIKIO:
Ni ndoto, ni ndoto, ni ndoto x 3
(ni ndoto)
Rudia x 4

Ubeti wa 1:
Hautapata rafiki kama mimi mimi ni msema kweli
Ndoto zinaweza kuwa za kweli au zisiwe za kweli
Lazima utazame mbali
Unapoota unapata haina maaana ndio unapata hata
Ni kitu ambacho ni sawa kula kwa macho
Kipi kikusikitishacho
Hakuna ajabu kwa wa kwanza kuwa wa mwisho
Maisha yanaambatana na vitisho
Huyu hatasema hivi kuhusu Yule na Yule atasema vile
kuhusu huyu hapa na pale na hii ni methali ya watu wa kale
Akuanzae mmalize wacha kusema sana
Wacha kuota ndoto za mchana
Kila mtu anaota ndoto maskini anaota ndoto kuwa tajiri
Na tajiri anaota ndoto kuwa tajiri zaidi
Ndipo dhuluma inapozidi
Na watu wengine wanauana inapobidi
Kila mtu anaota pesa yes hata Wanasiasa
Na haswa wanasiasa wa sasa

(Rudia Kiitikio)

Ubeti wa 2:

Chok.. ungefanya nini baba asingepata Ubunge
Ungeweza kukimbiza mbio za Mwenge
Maana una unachowaza cha maana
Sana sana unota ndoto za mchana
Unataka hiki na hiki Adidas mara Nike
Wakati kuangaika hutaki
Tukueleweje salama au walama
Sema kama hauna noma hapa ndiyo Darisalama
Na sisi ndiyo wasanii tunazungumza kisanii
Dizaini hii tuko wachache sana kwenye jamii
Tuna mawazo mazito na hatuamini sana ndoto
Na kama ndoto zote zingekuwa za kweli
Watabiri wangekuwa matajiri najaribu kufikiri
Wangewapata mpaka mawaziri wa serikali
Hakuna binadamu anayetosheka
Maisha yote ni mashaka
Kila mtu hawezi kupata kila kitu anachotaka
Ni ndoto na kucheza na maisha ni sawa kucheza na ndoto
Samahani ningependa kutoa wito
Vijana wavulana na wasichana
Tuendelee kukazana tu usiku na mchana
Hakuna kusema hapana
Daima mbele kurudi nyuma ni mwiko
Chok.. inakubidi ukubali mabadiliko
Usilete zako za 1947 1999
kila mtu anaota ndoto za pesa kisa kutesa
Nani atafanya makosa

(Rudia Kiitikio)

Usiku naota ndoto napigana na shetani
Mchana naota ndoto natoa hotuba bungeni
Mwaka 2000 Rais ni nani
Ni ndoto x 5

MWISHO

Kuanzia kesho tutakuwa tukiuchambua wimbo huu, toa maoni kuhusu mtazamo wako na unadhani msanii dhamira yake ilikuwa ni nini, maoni yako nk.
Uchambuzi utaongozwa na: Kwame Anangisye