Tuko Pamoja

Tuko Pamoja

Friday, August 8, 2014

SUGU AWALAUMU POLISI KURUSHA MABOMU MBEYA

Mbunge wa Mbeya mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ amelishutumu Jeshi la Polisi mkoani humo kuwa ndiyo chanzo cha vurugu baada ya juzi kutumia mabomu ya machozi kuwazuia wafuasi wa Chadema na waombolezaji kuubeba mikononi mwili wa Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Itiji,  Ezekiel  King kwa lengo la kutembea nao kwa miguu kutoka Hospitali ya Rufaa Mbeya hadi nyumbani kwake Itiji kuuzika.
Baada ya mabomu hayo kurushwa, viongozi na waombolezaji walilazimika kulibwaga chini jeneza la mwili wa marehemu na kuanza kukimbia.
Marehemu alifariki dunia katika hospitali hiyo, alikopelekwa  kwa ajili ya matibabu baada ya kuugua ghafla katika Gereza la Ruanda alikokuwa akitumikia kifungo cha miaka saba baada ya kupatikana na kosa la kudhuru mwili wa mwanachama wa CCM .
Akizungumzia tukio hilo, Sugu alisema kilichotokea juzi ni uthibitisho kwamba polisi ndiyo wamekuwa chanzo cha vurugu.
“Sisi tulikuwa kwenye msafara wakaja kutuzuia na kuninyooshea bunduki. Tukawaeleza tunakwenda kuzika, wao wanasema tulitakiwa kuomba kibali cha kwenda kuzika,” alisema Sugu na kuongeza: “Watu walikuwa wengi na magari ya kuwabeba kwenda kuzika hayakuwepo, tuliamua kutembea sasa kibali cha nini,” alisema Sugu.

Sugu alisema polisi wasipobadilika mara moja, wananchi watachukua hatua kuwaondoa katika nyumba walizopanga uraiani ili wakaishi kituo kikuu cha polisi mkoani humo kwa vile hawaijali jamii inayowazunguka.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Ahmed Msangi aliwataka Chadema kuacha kuwazushia polisi na kuongeza kuwa madai ya Sugu hayana ukweli wowote.
  • Mwandishi Wetu, Mwananchi

Thursday, August 7, 2014

MBUNGE JOSEPH MBILINYI AKABIDHI VIFAA VYA CHAMA KWA BAVICHA JIJINI MBEYA

  • KATIBU WA MBUNGE KWAME ELLY ANANGISYE AMKABIDHI MWENYEKITI BAVICHA MBEYA MJINI  MOSES MWAIFUNGA KWA NIABA YA MBUNGE 
 

POLISI MBEYA WAFYATUA MABOMU NA KUPORA JENEZA MBELE YA MBUNGE JOSEPH MBILINYI "SUGU"

  • NI LA MAREHEMU KING ALIYEKUWA MWENYEKITI  SERIKALI YA MTAA ITIJI
  • ALIFIA GEREZANI ALIKOKUWA ANATUMIKIA KIFUNGO CHA MIAKA 7
  • RUFAA YA KESI YAKE YENYE UTATA ILIKUWA ISIKILIZWE TAR. 11/8/2014


 
 
  •